
Paul Chrispin Mfungahema ni mmiliki na Mkurugenzi wa Shule ya Utoto, Shule ya Msingi, na Sekondari ya St. Rosalia ambayo ilisajiliwa mwaka 2014. Kwa kipindi cha miaka 3 sasa, LOLC Tanzania imekuwa ikifadhili St. Rosalia katika miradi yao kama vile kujenga hosteli, kununua mabasi ya shule, na kupanua shule. St. Rosalia bado inahitaji mikopo zaidi kutoka LOLC Tanzania.

Makata Abdallah ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mbugila Investment inayojihusisha na huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo. Amekuwa akijua LOLC Tanzania kwa zaidi ya miaka 3, na LOLC Tanzania alimsaidia kwa mkopo wakati biashara yake ilikuwa ndogo hadi sasa ambapo biashara imekua. LOLC Tanzania imemsaidia sana kupitia ufadhili.

Chichi Hussein Mfuko ni mfanyabiashara katika Kitumbini anayeuza nguo, na amekuwa mteja wa LOLC Tanzania tangu mwaka 2006. Amekuwa akipokea mikopo ambayo imesaidia biashara yake kukua. Mtaji wake umeongezeka na anaweza kulipa ada za shule na kusaidia familia. Ana himiza wanawake wengine kuchukua mkopo kutoka LOLC Tanzania.